Baraza la Mitihani nchini (Necta) limetangaza kuahirisha mitihani ya kidato cha sita na ualimu iliyokuwa ifanyike Mei 4 mwaka huu 2020 hadi pale itakapotoa taarifa mpya.

Hatua hiyo imekuja baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kutangaza Machi 17, kufungwa shule na vyuo vyote  ili kuondoa misongamano na kupambana na virusi vya ugonjwa wa corona.


Kupitia maagizo hayo Necta imetoa maelekezo kwa maofisa elimu wa wilaya kuwajulisha wakuu wa shule na vyuo vya ualimu nchini wawajulishe watahiniwa kuhusu kuahirishwa kwa mitihani hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post