Kuna watu nature yao wanapenda usafi, akiamka asubuhi atasafisha alipo lala, bafuni atakuweka sawa baada ya kutumia, jikoni ataweka kila kitu sawa baada ya kutengeneza kifungua kunywa. A tafuta vumbi TV kabla ya kukaa na kuangalia taarifa ya habari.

Mtu wa pili atakua na budget nzuri ya pesa. Ukimpa laki tano ya matumizi inaweza kumaliza miezi mitatu hajaomba hela na ukirudi kutoka kazini chakula utakikuta. Utagundua pesa imekwisha pale utakaporudi na kukuta dinner ya wali mchicha na ukimuuliza sana atakuambia ni mchele tunaomalizia na mchicha nimechuma hapo nyuma.

Hawa watu hata wakiwa na mabishano ya kawaida ya kibinadamu hawezi mmoja kulalamika kuwa mimi huwa ninasafisha bafu kila siku wewe hisafishi kwakua kusafisha bafu hajitumi. Au huyu wa pili hawezi kusema nimekuvumila tunakula wali na mchicha, kuweka hela ni jadi yake

Kuna wanaooa uzuri, msichana mrembo au mwanaume mwenye sura ya kuvutia siku ya kwanza tu ulimuona mapigo ya moyo yalikwenda mbio. Huyu hata akikuudhi ukishaona sura yake unatabasamu. Unawahi kufika nyumbani ili tu umuone.

Hii ni mifano tu, lakini usiombe uolewe au uoe asiyeelewa jitihada zako, kila unachofanya haridhiki. Huyo si soul mate.

Post a Comment

أحدث أقدم