Watu 350 wapimwa na kukutwa na virusi vya corona  katika mataifa 28 barani Afrika.
Benin na Tanzania zatangaza kesi yake ya kwanza kila mmoja tangu kunza kwa  janga hilo  mwishoni mwa mwaka  2019.
Bara la Afrika  hadi wiki iliopita ilikuwa bado imenusurika na virusi hivyo hadi kesi chache kuanza kuripotiwa .
Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO  limetangaza Jumatatu  kuwa barani Afrika katika mataifa 28 ni watu 350 ndio waliokutwa na virusi vya corona baada ya kupimwa.
Nchini Benin, mtu wa kwanza kukutwa na virusi hivyo ni mwanamume mwenye umri wa miaka 49  na raia wa Burkinafaso ambae aliwasili nchini Benin  Machi 12.
Tanzania imetangaza mtu wa kwanza kuwa na virusi hivyo  huku mataifa jirani yakitangaza pia kuchukuwa hatua zinazostahili  kuzuia kujipenyeza kwa virusi hivyo.
Mtu huyo aliekutwa na virusi ana umri wa miaka 46 aliwasili  nchini Tanzania akitokea nchini Ubeligiji Machi 15.
Rwanda imetangaza kesi 6 mpya  kwa muda wa masaa 48.
Wizara ya afya ya Rwanda amefahamisha kuwa mmoja miongoni mwa waathirika  ana umri wa miaka 30 na mkazi wa jiji la Kigali .
Afrika Kusini ndio taifa lililoathirika kwa kiasi kikubwa barani Afrika na wagonjwa 51 baada ya Misri yenye wagonjwa 126.
Rais wa Afrika Kusibi Cyrille Ramaphosa  ametangaza kusitishwa kwa safari kutokea katika mataifa yenye  tishio kubwa la Covid-19  kama Italia , Ujerumani, China na Marekani.

Post a Comment

Previous Post Next Post